Monday, June 7, 2010

Alikuwa bize kweli kweli...

Tulifika ktk moja ya picnic site iliyopo ndani ya crater (njiani kutoka nje) tulikutana na huyu tumbili ambae alikuwa yupo busy sana. Tulipofika hapo picnic site (ambapo sisi tulienda kuchimba dawa) tulikutana na jamaa wengine ambapo story zilianza na tukajisahau.
Kufumba na kufungua huyu tumbili akawa tayari yupo juu ya roof ya gari yetu ambayo ilikuwa wazi akijaribu kuzama ndani kuangalia chochote. Kelele za kuhamaki kwetu zilimshtua na akaachana na hiyo biashara. Licha ya kwamba ni mdogo kiumbo lakini alikuwa na jeuri ya kumdhihaki mdau mfawidhi wa Tembea tz kwa sababu tu alikuwa ni mwanamke ambae alikuwa ndani ya gari muda wote. Mimi na Guide tulikuwa nje ya gari na mbali kidogo tukijinyoosha na kuagana na jamaa tukliokutana nao hapo picnic site ambao walikuwa wanafahamiana na guide wetu.

Hakuishia hapo, akasogea pembeni na kuendelea na mishughuliko mingine.

Akijipanga upya baada ya jaribio lake kuzimwa. Hii ilikuwa ndani ya hifadhi ya Ngorongoro crater.

No comments:

Post a Comment