![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhShGdqJOSRJ0v_OfIU2h-B88bHccG2hoTRxJ02TsZcUKIUtSuKn-y1bwanvMjqcCSf-2Qywngknauu0PIlvm4eMHZ4SPilSecjlZYhoJ4PIW8-ZLw4mVplp5kFeykjdFhlc1JyLwwAx5Le/s400/01.jpg)
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhRfKjumNII5YFGwpNvl9WmdD-ENDJq9wLnUu7wYXzryROLI1N4pTF3CFaoGL6bTOB-h6cv6hr0MqOnK-2Rd4msK_4BCy_kxXP_19xLoY_hyFC4UxqV8Vbh07nt9-Tc9F-YZVBTzTgaBIxd/s400/02.jpg)
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhHtMHkxVbNDscRd9EVgjYh8fo8UJWlDAGs4f1SbvDxuzwK2XMIPjwcGoefsSVxpjuAlSEuwebx5rg9C_DBo_5jvad4m4f1sl4B5YwAG3TlLQyMGKJrz4qCMmtUTDp_wzEUWbUZfbxJwIiu/s400/03.jpg)
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgsW_MIS5WvGaVt7ivddpHpPRY5IrIZgu924uJ0MoBmGR9XVhy-MEORv6jxeAokZpKAnfbs7851fj2W0cPEeGdDKtHKeq6GQcBVNqgN1hkCBgdeWyIT0PHv-KgIZJZP2oElSyOlKkM7hDKk/s400/05.jpg)
Kuna dondoo moja nilipewa nilipokuwa Serengeti mwaka jana ni kwamba endapo nyumbu wa kwanza atavuka mbele ya gari lako. Basi nyumbu walio nyuma yake nao watataka wapite mbele ya gari lako na sio nyuma hata kama gari limesimama. Tena hali huwa mbaya zaidi kama utakutana nao usiku ukiwa umewasha taa za gari yako. Wote watataka wapite mbele ya gari yako (kwenye taa). watafanya hivyo hata kwa kulikimbiza gari lako sambamba hadi hapo utakapochochea zaidi. Na hata ukimpita, atasimama atafakari nini cha kufanya.
ha ha ha ha, kweli Nyumbu ndivyo walivyo, huwa wanashangaa sana kama vile akili zao zimewapotea ghafla au zimepungua wanasubiri zijae ndipo wawaze. Nimecheka sana hawa wapangaji hawatulii, kazi wenda na kurudi tu.
ReplyDelete