Friday, December 10, 2010

Lagoon Walk, Ras Kutani (2)

Baada ya kutua, wageni huchukuliwa na magari toka Airstrip hadi kuletwa eneo hili. Hapa hushuka na kisha kuteremka bondeni ambako ilipo Lagoon. Baada ya kufika Lagoon wageni hupanda boti ambayo huwafikisha hadi hotelini. Airstrip ya Ras Kutani ipo mbali kidogo na eneo hili.

Kwa mbali ni bahari ya hindi na ngazi zinazoshuka chini ni ngazi zinazoelekea ilipo lagoon.

Hapa wageni hupanda boti na kisha kusafirishwa mpaka ilipo hoteli ya Ras Kutani. Kwa hapo Hoteli ipo upande wa pili wa Lagoon.

Ngazi zinavyooneka tokea kwa chini. Eneo linapoishia magari lipo juu ya kilima.

Safari ya boti huishia kwenye hicho kibanda kinachooneka. na boti unayoiona mbele ya hicho kibanda ndio boti inayotumika kwa shughuli za kusafirishia wageni kati ya hoteli na upande wa pili wa Lagoon kuelekea kwenye kiwanja kidogo cha ndege cha Ras Kutani.

Sababu kubwa ya hoteli hii kumiliki uwanja wake wa ndege licha ya kwamba ipo karibu na dar ni kurahisisha usafiri kwa wageni wake baina ya Ras Kutani na hotel nyinginezo. Ras Kutani inamilikiwa na kampuni ijulikanayo kama Selous Safaris kampuni ambayo inamiliki hoteli nyingine 2; Jongomero (Ruaha NP) na Selous Safari Camp (SelousGR). Wengi wa wageni (hususan wanaotoka nje ya nchi) huandaliwa mpango wa kutembelea Ruaha na Selous ambako hukaa ktk hoteli zilizo chini ya kampuni ya Selous Safaris. Mara nyingi safari zao huanzia ktk hifadhi na mwisho wa safari kabla ya kurudi makwao, wageni huja Ras Kutani kupumzika ktk pwani hii na kuondoa uchovu wa safari za porini. Ili kuwapunguzia muda wa safari, kampuni ya Selous imeweka viwanja vya ndege ili wageni waweze kusafirishwa kirahisi toka hifadhi moja kwenda nyingine na mwishowe Ras Kutani kwa njia ya anga. hii haikuzii wewe mdau ambae unataka kwenda Ras Kutani kwa usafiri wako binafsi bila ya kutembelea maeneo mengine. Jambo la msingi ni kuhakikisha ya kwamba unafanya booking yako mapema kupitia wakala wako au kwa kutumia taarifa zilizopo ktk tovuti ya Selous Safari Company. Kwenye kila hoteli, tembelea sehemu ya gallery ujionee taswira maridhawa za kutoka ktk camp husika.

1 comment: