
Inaelezwa kwamba kinachotofautisha mbinu za kulinda na kuyahifadhi salama mayai ni rangi ya yale mayai yenyewe. Ki ukweli, Ndege au mnyama ambaye mayai yake yana rangi nyeupe, hutumia nguvu zaidi ili kuyalinda mayai yake kwa kuwa yanaonekana kirahisi sana. Ndege au mnyama huyo hufikia hatua ya kujenga kiota ktk mti eneo ambalo ni mbali na waharibifu wa mayai yao - wanyama wengine, nyoka na hata binadamu. Mamba hujenga kiota chake nje ya maji lakini huhakikisha amekifukia vizuri na zaidi ya hapo huweka lindo madhubuti ili eneo husika lisisogelewe na mharibifu yoyote yule.
Wale ambao rangi ya mayai yao si nyeupe, wao huwa hawana wasiwasi sana wa kuyaficha mayai yao. wao watataga mayai yao sehemu ya wazi na kisha kuyaacha hapo bila ya kuchukua hatua za ziada kuyaficha. hii inatokana na imani yao kwamba si rahisi mayai yao kuonwa.
No comments:
Post a Comment