
Mkeka unaoanza nao ferry unaendelea kwa sehemu kubwa ya safari yako. hapa ni mitaa ya Gezaulole njiani kuelekea Ras Kutani. Ras Kutani ipo eneo lijulikanalo kama Gomvu

Mkeka unapofikia tamati utasonga na barabara ambayo imeshindiliwa vizuri na kufanya safari yako kuendelea bila ya purukushani au kuwa na haja ya kutumia 4x4

Safari inaendelea, ukiachana na barabara iliyoshindiliwa unaingia kwenye hizi barabara ndogo ambazo nazo hali yake ni nzuri kama uonavyo

Nilihisi kama nipo mbugani kwa jinsi mandhari ya njiani yanavyoshabihiana na yale ya porini.
kazi nzuri KK
ReplyDelete