Porini, viboko wanajulikana kwa kuacha alama zinazoonyesha mapito yao. hufanya hivi kwa kuacha kinyesi ktk sehemu muhimu za mapito yao ili wasipotee wakati wa kurudi. Ukitembelea hifadhi ya Selous na kufanya walking safari pembezoni mwa mto Rufiji utajionea hali halisi ya hizi alama kando kando ya mto. Licha ya kuonekana ni kibonge, kiboko ana uwezo wa kutimua mbio kumzidi mwanadamu.
Ni Mnyama wa porini anaefahamika sana kwa kuwa na hasira na ndie anaeongoza kwa vifo vingi vya binadamu vinavyotokana na kushambuliwa na wanyama wa porini. Picha juu ilipigwa pembezoni mwa mto Ruaha, ndani ya hifadhi ya taifa ya Ruaha. Shukran kwa mdau Tom, Kima safaris
No comments:
Post a Comment