![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEg9YfJ8rXbKapCR8LWK_o3BFb87VLyC8-1A7bXKrn8cXDH1RWifmB12PYVebO0x41PJ2308TITo2mob0vTIcPtoHqFmzBH2WGaDwXrhII0IcgLXb2nluVwO2AYi5lzJTMpn0HJiSlcvWuS3/s400/01.jpg)
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhP0maVwfqL5j9yJ_h8npk7ItQQz9BRuoDdQbW4ZUcNvT1gS33c_KhdgTasBplFq5072BoGMbb9RiYzbkdlRdgzzkkn5CnjqqWydMp8_K9OyKhRoOH2g35a1ri9TSJW1HVVF-zYJfkcKt8U/s400/02.jpg)
Picha hii inaonyesha mandhari ya Bwawa la Kuogelea la hotel ya Kilimanjaro Kempinski Dar-Es-Salaam. Baada ya kufanyiwa ukarabati, Bwawa la kuogelea la hoteli hii lilihamishiwa ghorofani badala ya kule nyuma lilipokuwepo awali. Nadhani wadau wa disko la enzi hizo la pool side mnalikumbuka eneo lenu la matukio vyema! Enzi hizo hotel hii ikijulikana kama Kilimanjaro Hotel na kumbi yake maarufu ya mikutano iliyojulikana kama Simba Grill.
Mimi nalikumbuka sana lile bwawa la zamani la kuogelea kwani weekends (wakati nipo Shuleni) nilikuwa sikosekani hapo kupiga mbizi na wadau kadhaa tuliokuwa tukisoma wote. Ahsante ya picha-TTB.
No comments:
Post a Comment