Saturday, May 4, 2013

Unavyoviona ukiwa Horombo Hut

TPC Sugarcane plantations
 Kituo cha Horombo, ni moja ya vituo ambavyo mgeni anakuwa anapata view nzuri ya jiji la Moshi, maeneo yake na baadhi ya vitu vilivyo ndani ya mkoa wa Kilimanjaro. Hali ya hewa ikiruhusu (hususan mawingu) ukiwa Horombo unauona mji wa Moshi vyema na usiku taa za jiji hilo zinaonekana vyema. Nyakati za usiku, taa za uwanja wa ndege wa Kilimanjaro huonekana na kama kuna ndege zinazoruka na kutua zinakuwa zinaonekana pia. Taa za maeneo ya Boma Ng'ombe na maeneo jirani huonekana pia. Picha juu ni mashamba ya miwa ya Kiwanda cha sukari cha TPC Moshi yakionekana.

TPC Sugarcane plantations
Mashamba ya TPC yakionekana kwa mbali kidogo

Lake JIpe
Ziwa Jipe, ziwa hili lipo kwenye mpaka wa Tanzania na Kenya

Nyumba ya Mungu Dam
Bwawa la Nyumba ya Mungu nalo linaonekana

Nyumba ya Mungu Dam
Milima ya Upare nayo inaonekan hususan safu ya kaskazini

No comments:

Post a Comment