Friday, February 8, 2013

ATCL yazindua safari zake za Dar - Mtwara

ATCL Mtwara
Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) leo Februari 8, 2013 limerjesha huduma zake kati ya miji ya Mtwara na Dar Es Salaam. Ndege ya Shirika hilo aina ya Dash 8 iliondoka Dar hii leo na kutua mchana na kupokelewa na baadhi ya wananchi wa mji huo. Picha juu ni ndege hiyo iliyotumika kwenye uzinduzi wa safari hii ikiwa inapakia abiria katika uwanja wa Julius Nyerere Dar Es Salaam.

ATCL Mtwara
Captain Richard Shaidi (Kushoto) akiwa sambamba na msaidizi wake wakiwa hewani njiani kuelekea Mtwara hii leo wakati wa uzinduzi wa safari kati ya Dar na Mtwara

ATCL Mtwara
Safari kuelekea Mtwara ikiendelea

ATCL Mtwara
Huko Mtwara nako kulikuwa na hafla fupi ya uzinduzi iliyofanyika katika uwanja wa ndege wa Mtwara

ATCL Mtwara
Jengo la uwanja wa Ndege wa Mtwara

ATCL Mtwara
Ndege hii iliondoka Dar ikiwa na Mruko namba TC116 na kisha kurejea kama TC117.
Picha zote na taarifa toka ktk ukurasa wa Facebook wa Air Tanzania.
Ungana nao ili ueweze kupata taarifa zaidi kuhusu huduma na mambo mengineyo kuhusu ATCL

No comments:

Post a Comment