
Ibrahim A. Mussa (53) ni mtumishi wa Wizara ya Maliasili na Utalii tangu mwaka 1982 hadi sasa ambapo alifanya kazi katika ngazi mbalimbali, katika Idara ya Misitu na Idara ya Utalii. Kabla ya kuteuliwa kuwa Mkurugenzi wa Utalii, Ibrahim A. Mussa alikuwa Mkurugenzi Msaidizi anaesimamia Utafiti, Takwimu na Mafunzo katika Idara ya Utalii.
Bw. Mussa ana Shahada ya Uzamili (International Tourism Management) aliyoipata mwaka 2005 kutoka chuo cha Sheffield nchini Uingereza. Bw. Mussa anachukua nafasi ya Mkurugenzi wa Idara ya Utalii kutoka kwa Bi. Maria Mmari ambaye amepangiwa kazi nyingine.
No comments:
Post a Comment