
Katika kundi la watu walioanza kufikiria namna ya kuwalinda wanyama hawa (na wengineo), nimefurahishwa na comments alizotoa Paul James wa Clouds FM ktk kipindi cha power breakfast leo asubuhi.
PJ (kama anavyojulikana na wengi) alisema kwa kuwa Pembe za Faru zinatumika (mashariki ya mbali na Asia) kuwasaidia watu wenye matatizo ya 'Jogoo kushindwa kupanda mtungi', kwanini nchi hizo wasipewe namna mbadala ya kushughulikia tatizo hilo kwa kutumia miti shamba ambayo ipo kwa wingi hapa nchini na kwengineko? PJ alienda mbele kwa kutaja jina la Mkuyati, mti/dawa ambayo inaelezwa ya kwamba inawasaidia watu wenye shida hizo na kuleta hali ya bendera chuma, mlingoti chuma..
japo comments zake zimekaa kimzaha mzaha, lakini ni jambo ambalo linaweza kuangaliwa ili kutokomoze mauaji haya. Swala hili linahitaji kuunganisha nguvu za pamoja baina ya wahifadhi wa wanyama pori, wataalam wa misitu, wataalamu wa afya(hususan maswala ya Jogoo kushindwa kupanda mtungi) ili kuweza kupata suluhu. Si vibaya kuliangalia hili kwa mtizamo huu
No comments:
Post a Comment