Thursday, March 25, 2010

Dar Es Salaam Zoo...

Ikiwa wewe ni mpenzi na mnazi wa mambo ya wanyama pori lakini unakosa muda wa kwenda porini kutembelea na kuwaona wanyama wakiwa ktk mazingira yao, Dar Es Salaam Zoo inakupa nafasi ya kuwaona wanyama wakiwa ktk Zoo hii. Dar Es Salaam Zoo ipo maeneo ya kibada, Kigamboni nje kidogo ya jiji letu. Ni Sehemu murua kutembelea na familia na kujionea wanyama na ndege mbalimbali. Timu ya TembeaTz iliwahi fanya ziara yake maeneo haya mwishoni mwa mwaka jana. Picha juu ni ndege aina ya Marabou Storks ambao na wapo DSM zoo. Wadau wanaoishi kando kando ya ziwa Victoria (maeneo yenye shughuli za uvuvi) wanawaelewa hawa ndege.

Wana collection ya ndege mbalimbali wa porini ambao wanawekwa ktk banda moja, hapo utawakuta Flamingo, Egyptian geese, aina mbalimbali ya Storks, Hornbills, Bata mzinga na kadhalika.

Mfalme wa Jangwa nae yupo kwa sana ndani ya DSM zoo.

Kama kawa, mkusanyiko wa wanyama pori bila ya uwepo wa sharubu haunogi. Sharubu nae yupo, tena dume.

Wa Juu (chui) nae yupo kuwakilisha

hilo ni banda la nyani na ngedere.

Ukitaka kupanda ngamia kazi kwako, huduma hii ipo pia DSM zoo.

http://daressalaamzoo.com/index.htm

No comments:

Post a Comment