![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEi4hw6IVXS_dT8Gfxn9qC_ef1_fKchMGBPS0-vx3kgkAvbihjtIWzMFL-6SobYU0KXiZKWmFFK7MA9iRklNUugIOrflEi7e5OdCkWSA6uo_1cvIpXRJaj3gHWgIKSNXx3GDf056HxyzW0BQ/s400/pics01+803.jpg)
Siku mbili baadae wakati tukiwa tunazunguka ktk maeneo ya hoteli tulimuuliza mmoja wa wafanyakazi kuhusu chui huyu ambae tulimuona chini ya kilomita mbili toka ilipo hoteli. Mfanyakazi yule alitujibu kuwa wa juu huyo yupo ktk teritory yake na huonekana mara nyingi sana na wageni maeneo hayo. Hususan mida ya jioni, mida ambayo na sisi tulimuona pia. Akasema kipindi cha kiangazi kinapogonga hodi, wa juu huyo hujongea maeneo pembeni ya bwawa la kuogelea la hoteli kwa lengo la kunywa maji toka ktk bwawa hilo mida ya usiku. Tulishukuru mungu kujua hilo siku ambayo kikosi kazi cha TembeaTz kilikuwa kina-check out ktk hotel na kuendelea na shughuli ktk mbuga nyingine.
No comments:
Post a Comment