Picha juu ni Barabara iendayo Tunduru toka Songea Mjini, hapo ikiwa ni katika eneo liitwalo Mahenge (sio ya Morogoro). Mahenge ni kama Oysterbay (DSM) au gangilonga (Iringa) kwa Songea Mjini.

Moja ya Viongozi aliyepata kuongoza taifa letu aliwahi kusema, nanukuu
"ukiona mtanzania anazungumzia ukabila au eneo analotoka, basi ujue huyo anajaribu kuwatafuta watani zake na si kwa nia ya ubaguzi".
Nina imani kubwa sana kwa mtundiko huu, watani zangu wengi sana watajitokeza.
Nimebahatika kutembelea nchi moja jirani (ankal hupenda kuiita - watani wa jadi) na kuona hali ya ukabila ilivyoshamiri huko. Ukabila unapopewa kipaumbele kwa nia ya kubaguana ni jambo la hatari ambalo namshukuru mungu ametuepusha nalo mbali kwa kiasi cha kuridhisha hapa kwetu.
hii leo watu ambao si wazaliwa wa eneo fulani wanaweza kugombea uongozi na ktk maeneo ambayo si chimbuko lao. Kama ukabila ungekuwa umeota mizizi hapa kwetu, ni dhahiri wabunge wengi wa majimbo ya hapa Dar wasingeupata ubunge kwani wengi ni wahamiaji. - sio wazaliwa wa hapa jijini. Hili ni jambo la kujivunia na hatuna budi kuliendeleza hususan ktk kipindi hiki ambacho joto na pressure ya uchaguzi inaanza kupanda taratibu.
"ukiona mtanzania anazungumzia ukabila au eneo analotoka, basi ujue huyo anajaribu kuwatafuta watani zake na si kwa nia ya ubaguzi".
Nina imani kubwa sana kwa mtundiko huu, watani zangu wengi sana watajitokeza.
Nimebahatika kutembelea nchi moja jirani (ankal hupenda kuiita - watani wa jadi) na kuona hali ya ukabila ilivyoshamiri huko. Ukabila unapopewa kipaumbele kwa nia ya kubaguana ni jambo la hatari ambalo namshukuru mungu ametuepusha nalo mbali kwa kiasi cha kuridhisha hapa kwetu.
hii leo watu ambao si wazaliwa wa eneo fulani wanaweza kugombea uongozi na ktk maeneo ambayo si chimbuko lao. Kama ukabila ungekuwa umeota mizizi hapa kwetu, ni dhahiri wabunge wengi wa majimbo ya hapa Dar wasingeupata ubunge kwani wengi ni wahamiaji. - sio wazaliwa wa hapa jijini. Hili ni jambo la kujivunia na hatuna budi kuliendeleza hususan ktk kipindi hiki ambacho joto na pressure ya uchaguzi inaanza kupanda taratibu.
No comments:
Post a Comment