
Picha juu niliipiga nikiwa ktk treni maalum ya TAZARA mwaka jana mwezi wa saba (kipindi cha Sabasaba). Ilikuwa ni treni mahususi kwa ajili ya utalii. Mnapanda pale TAZARA Station na kuelekea Stand ya Kisaki. Mkiwa njiani treni hupitia pori la akiba la Selous ambako baada ya kuingia ndani ya Hifadhi, Treni hupunguza mwendo ili kutoa nafasi kwa abiria kuona wanyama watakaoukuwepo pembezoni mwa reli. Ni nafasi nzuri pia kujionea wanyama na pori la Akiba la Selous. TAZARA huwa na hizi safari kila mwaka wakati wa kipindi cha sabasaba.
No comments:
Post a Comment