Thursday, April 15, 2010

hula majani akizidiwa....

Inaelezwa ya kwamba sharubu hula majani (japo si kwa kiasi kikubwa kama swala au nyumbu) pindi mambo yanapomuendea sivyo ndivyo. Hufanya hivi baada ya kula nyama ambapo majani hizo huenda kutuliza munkari wa acid zilizopo tumboni mwake zisishambulie tumbo lake. pia hula majani kama atakuwa hajapata chakula muda mrefu sana. hii inamsaidia kwenda kuzuia acid hizo kulishambulia tumbo lake ambalo wakati huo linakuwa tupu. yawezekana wengi waliomshuhudia sharubu akila nyasi, ni ktk kipindi ambacho Sharubu anakuwa 'amezidiwa' - hajala.
Paka na mbwa nao wanatabia hizi pia. picha ni sharubu akiwa ndani ya hifadhi ya taifa ya Ruaha national Park.

Angalizo:
Mtundiko huu hauna uhusiano wowote na mtanange baina ya watani wa jadi unaotarajia kufanyika weekend hii.

1 comment:

  1. Ha ha ha ha.... hii ya kujitoa kwenye u-simba na u-yanga nimeipenda.

    ReplyDelete