Wednesday, November 28, 2012

Vijimambo vya kwenye Walking Safaris hapa Tanzania

Tanzania Giraffe Safaris Limited
Soma zaidi kupitia Tanzania Giraffe Safaris Ltd

Bongo kuna Tambarare na Milima.....

Unaweza kubashiri hapa maeneo yepi ndani ya nchi yetu?

Taswira za Ruaha NP






Shukran kwa mdau Rajab wa Wildness Safaris

Singita Mara River Tented Camp

We are thrilled to share the first pictures from our brand new camp, Singita Mara River Tented Camp, situated in the Lamai triangle, the northernmost tip of the Serengeti National Park in Tanzania. The camp offers a pared-down approach to the quintessential Singita safari without compromising on any creature comforts.

Singita’s philosophy of preserving iconic locations by offering ‘fewer beds in larger areas’ is epitomised by Mara River Tented Camp’s remote position in the Lamai triangle – with only 16 beds surrounded by 98,000 acres of untouched wilderness.  It is a wildlife viewing area with abundant year-round concentrations of resident plains game, big cats and elephant in addition to the Mara River’s large populations of crocodile and hippo.

Read More from Singita Blog

Friday, November 16, 2012

Something to know about FastJet....

Africa's low-cost airline…

With ambitious plans to create Africa’s first pan-continental airline, fastjet will bring international standards of safety, quality, security and reliability.
Low-cost is quite simply the avoidance of costly frills, offering customers the lowest possible fares in addition to pay-as-you travel extras. This affords passengers the flexibility to pay for additional services such as a bag or refreshment rather than having to pay for it regardless whether you want it or not.

How your travel arrangements may look...


Importantly fastjet low-cost definitely does not mean low quality. Despite the many challenges that exist outside our control we will be open, honest, transparent and communicative to ensure that your travel arrangements remain with the least amount of interruption.

Our philosophy is that air travel should be easy…

  • Flights can be booked online, on a mobile phone, at one of our local travel agents or with one of regional sales offices
  • All will be supported by a choice of payment methods
  • www.fastjet.com will be the one website for Africa’s travel needs offering an increasingly wider choice of travel options
  • The best fares available online and in KSh, TSh and USh
  • You can manage your own booking, changing the date of travel (at extra cost) and choose your seat (coming soon..)

We believe our people make a world of difference…

Alongside our service orientated regional teams, trained to offer the highest levels of customer service and the aircrew, we have assembled an international management team steeped in low-cost airline management, engineering and operational expertise.

We look forward to welcoming you onboard…

Chanzo: http://www.fastjet.com/tz/our-airline

Jioni moja huko Selous Game Reserve










Thursday, November 15, 2012

Drogba wa Selous (Mloka) akiwa mzigoni



Ni kwenye mapori yaliyopo ktk kijiji cha Mloka, nje ya Pori la akiba la Selous huko Rufiji.

Mwananyika aka Drogba wa Mloka, Selous Game Reserve

Selous Game Reserve
 Ni Mjasiriamali aliyewekeza nguvu na uelewa wake wa mambo ya wanyama pori na mazingira yao kwa kuwaelimisha wageni wanaungana nae. Hujulikana kama Mwananyika lakini hivi karibuni amepewa jina la Drogba (wanadai ya kuwa kafanana na Drogba yule mwanasoka maarufu). Anapatikana kwenye kijiji cha Mloka huko Rufiji, kijiji ambacho kipo nje ya pori la akiba la Selous.

Selous Game Reserve
Shughuli yake kubwa inayompa ugali wake ni kuongoza wageni kwenye safari za matembezi. Mwenyewe hujigamba kwa kuziita true Africa walking safari. Daima anapokuwa mzigoni huwa anavaa mavazi ya asili kabisa ambayo kayatengeneza kwa magome ya miti huku akiwa amebeba ngao, mkuki na kikapu chake cha kuobebea mitishamba.

Selous Game Reserve
Safari zake huwa zinafuata barabara na wakati mwingine huacha barabara na kuingie mapori. yeye huzunguka na wageni wake nje ya hifadhi japo pia wanyama wa porini (wakali na wapole) wanakuwepo. Kwa ajili ya tahadhari na usalama, anapofanya safari za miguu na wageni wake daima huwa anaambatana na askari toka kwenye campsite waliofikia wageni wake ambaye huwa na bunduki kwa ajili ya tahadhari. Angalia picha ya pila juu, upande wako wa kushoto utamuona askari mwenye riffle. Elewa ya kwamba safari za matembezi ndani ya hifadhi, mgeni husindikizwa na Ranger wa Maliasili na guide wake au ranger peke yake. Drogba yeye anacheza nje ya hifadhi.

Selous Game Reserve
Safari zake huwa na vituo vingi ndani yake na kwenye kila kituo kuna jambo ambalo huona ni vyema wageni wake wapate kulifahamu. wakati mwingine mkiwa nae safarini mnaweza kukutana na wanyama na wakati mwingine safari zake zikawa ni mafunzo ya wanyama na mazingira yao zaidi.

Selous Game Reserve
Mgeni hufundishwa namna ya kutambua nyayo za wanyama mbalimbali ambazo huwa wanakutana nazo wakiwa safarini.

Selous Game Reserve

Selous Game Reserve
Safari ikiendelea na vituo vikiwemo ndani yake

Selous Game Reserve
 Ahsante ya picha Mdau Rajab - Wildness Safaris Tanzania

Bwawa la viboko Mikumi NP

Mikumi National Park
Limezoeleka zaidi kama Bwawa la Viboko la Mikumu lakini ndani ya bwawa hili kuna zaidi ya viboko. Mamba nao wanapatikana kama jinsi ambavyo 'bango' linavyoonyesha na picha zinazofuata. Hapa wageni wanaruhusiwa kushuka kwenye magari yao na kujinyoosha. pia ni sehemu ya kupatia maakuli japo hakuna meza. Kwa ajili ya kupata maakuli wageni watalazimika kula chakula chao kwenye magari.   





 
Mikumi National Park
Bango liliopo pembeni ya Bwawa hili likitoa maelekezo ya muhimu kwa wageni na mambo ya kuzingatia wanapokuwepo hapo. Usafi ni moja ya mambo ya msingi ambayo mgeni anapaswa kuyazingatia anapokuwepo hapa na sehemu nyingineza ndani ya hifadhi.

Mikumi National Park
 Hawa jamaa ndio wanyama wa porini ambao wanaoongoza kwa kuuwa watu wengi barani Africa (Sub Sahara Africa). Kikubwa ni ukali wao ktk kulinda himaya zao ambazo zipo kwenye mito. Wengi wanaokumbwa na mikasa ya hawa majamaa ni wavuvi au watu wanaoenda kwenye mito na mabwawa kwa shughuli za kuchota maji au kufua

Mikumi National Park
 Porini wamepewa jina la Mkasi.

Mikumi National Park
 Huyu alikuwa nje ya bwawa akiota jua ili apandishe joto la mwili asiwe goigoi. Hawa ni wanyama wenye damu baridi, hutegemea joto linalopatikana kwenye mazingira ili walitumie kupandisha hali ya joto la miili yao. Wasipofanya hivyo huwa magoigoi hali ambayo huwaweka ktk wakati mgumu wa kujitafutia chakula.

Mikumi National Park
 Unaweza kupata uwiano wa ukubwa wake wa mwili sambamba na mazingira aliyopo. Bwawa linaonekana dogo lakini mamba wanaoishi humo ni wakubwa vya kutosha.

Mikumi hippo Pool
Ni ndiga ya Mdau Rajab wa Wildness Safaris Tanzania aliyekuwa huko mikumi hivi karibuni na kuturushia picha.

Gharama za Kutalii Gombe kwa raia wa Afrika Mashariki

Gharama halisi kwa mtalii yeyote wa ndani awe Mtanzania au raia nchi zinazounda Afrika Mashariki:

Kutoka Kigoma mjini kwenda Hifadhi ya Taifa ya Gombe kwa usafiri wa boti ya abiria ni Tsh. 4,000
Kuanzia Gombe kurudi mjini ni Tsh. 4,000.
Usafiri huu unapatikana siku zote isipokuwa Jumapili tu.
Muda wa boti kuondoka ni saa 6:00 (saa sita kamili mchana).
Ni usafiri salama tofauti na watu wanavyofikiria.
Ukifika Gombe wafahamishe kuwa nashukia Kasekela ( special area for tourism activities).
Hakuna usafiri wa kwenda na kurudi siku hiyo hiyo isipokuwa kwa ukodi boti binafsi ambazo ni gharama zaidi.

Ukifika Gombe utalipia TSh. 1500 kama  kiingilio (entrance fee) na TSh. 500 kama fedha ya kutembea (trekking fee) kwa siku moja. Utapata huduma ya malazi kwa kulipia kwa kichwa na si chumba, yaani mtu mmoja atalipia TSh. 5,000 tu kwa usiku mmoja, kama mpo wawili na mkatumia chumba kimoja mtalipia TSh. 10,000 tu kwa usiku mmoja pia. Gharama ya chakula ni TSh. 5,000 kwa mlo mmoja. Gharama ya vinywaji ni TSh. 1,500 kwa soda na 2,500 kwa bia.

Kumbuka: Unakuja Gombe kwa boti ya abiria, utafika mchana, siku inayofuata utafanya utalii na siku ya tatu utapanda boti hilo linalopita Gombe saa moja kamili ya asubuhi. Hivyo ni vizuri ujiandae kwa malipo ya nights 2 na milo ya siku 2. Kwa mtu asiye na mambo ya luxury sana akijipanga na TSh. 50,000 tu itatosha na chenji itarudi.

Watoto chini ya miaka 15 hawaruhusiwi kwenda kutalii bali watabaki rest house kwa usalama wa kutosha.

KARIBUNI SANA ndugu!

Monday, November 12, 2012

Precision Air becomes first airline to operate ATR 42-600 aircraft globally

Precision Air ATR 42-600
The ATR CEO Filippo Bagnato (right) shows the Precision Air Tanzania Chief Executive Officer Alfonse Kioko (left) the cockpit of the new ATR 42-600 aircraft purchased by his company during the official delivery of the aircraft at the ATR Delivery Center in Toulouse, France at the weekend.

Precision Air ATR 42-600
The ATR CEO Filippo Bagnato (left) shows the Precision Air Tanzania Chief Executive Officer Alfonse Kioko (right) the interior décor of the new ATR 42-600 aircraft purchased by his company during the official delivery of the aircraft at the ATR Delivery Center in Toulouse, France at the weekend

Precision Air ATR 42-600
The Precision Air Tanzania Chief Executive Officer Alfonse Kioko (first) and the ATR CEO Filippo Bagnato disembark from the ATR 42-400 aircraft after inspection of the plane’s facilities during the official delivery of the aircraft at the ATR Delivery Center in Toulouse, France at the weekend.

Precision Air ATR 42-600
The Precision Air Tanzania Chief Executive Officer Alfonse Kioko (left) receives keys for the company’s newly acquired ATR 42-600 aircraft from the ATR CEO Filippo Bagnato(right) during the official delivery of the aircraft at the ATR Delivery Center in Toulouse, France at the weekend

Precision Air ATR 42-600
Precision Air Tanzania and ATR staff pose for a group photo in front of Precision Air’s new ATR 42-600 during the official delivery of the aircraft at the ATR Delivery Center in Toulouse, France at the weekend.

Precision Air ATR 42-600
The Precision Air Tanzania Chief Executive Officer Alfonse Kioko (centre) toasts with the ATR CEO Filippo Bagnato (left) and the Precision Air Tanzania pilot Captain Itosi Marealle (right) during the official delivery of the ATR 42-600 aircraft at the ATR Delivery Center in Toulouse, France at the weekend

Thursday, November 8, 2012

Mdau Atembelea Hifadhi ya Kisiwa cha Saa nane Mwanza

Ni Mdau Abdul wa Respect Djs ambaye alitenga muda wake na kuamua kutembelea kisiwa cha saa nane kilichopo ktk jiji la Mwanza.

Tumbili wapo wa kutosha tu kisiwani hapo.

Ofisi za wasimamizi wa hifadhi ya Taifa ya Saa Nane. Awali kisiwa hiki kilikuwa ni hifadhi lakini mwanzoni mwa mwezi wa Tisa mwaka huu, Bunge limekipandisha hadhi na kukifanya kisiwa hiki kuwa Hifadhi ya Taifa na kuwa chini ya usimamizi wa TANAPA.

Kisiwa cha Saa nane kinafikika kwa njia ya boti tokea jiji la Mwanza. Boti inayoonekana juu ndio iliyompeleka Mdau Abdul mpaka Kisiwa cha Saa Nane tokea Mwanza mjini.

Mdau Akiwa kwenye boti tayari kwa kuanza safari kuelekea Kisiwani. Hapa ni akiwa upande wa Mwanza mjini





(Picha kwa hisani ya mdau Abdul wa Respect Djs)